Inawezekana ulijua tu mboga tunakula hutusaidia kujenga mwili na kutukinga dhidi ya maradhi lakini mboga za majani aina za ‘Spinach’ zinauwezo wa kipekee zaidi kwani zinaweza zikatumika kugundua mabomu.
Wanasayansi wameweza kuifanya mboga ya aina ya Mchicha au ‘Spinach’ kugundua bomu. Katika utafiti uliofanywa na wanasayansi wa MIT wamegundua kwamba … majani ya mchicha yanaweza kuhifadhi kemikali aina ya ‘Nitro-aromatics’ ambazo hupatikana kwenye mabomu ya kutegwa arthini na silaha zinazozikwa ardhini
Si lazima mboga hii iwekwe nyaya yoyote ili kuweza kugundua bomu bali vikompyuta vidogo ‘nanocomputers’ zinazowekwa kwenye mmea huo vitaweza kupata taarifa kama kuna madini yaliyonyonywa kupitia mizizi yake na kuyatambua kama ni ya bomu..kisha taarifa itatumwa kwenda kwenye kifaa kama simu au kompyuta ya mtu kwa kutumia mfumo wa WiFi au Bluetooth.
Jinsi utafiti huo ulivyofanyika
Wanasayansi waliweka kemikali za Carboni kwenye maji na kisha kufanya mizizi ya mboga kupitisha maji yale hadi kwenye matawi ya mchicha. Kisha wanasayansi wakapapasa majani ya mchicha kwa kutumia vyuma maalum na majani yale yalianza kutoa chembechembe za moto ambazo zinaweza kuonekana kwa kompyuta.
Pia chembechembe hizo zinaweza kuonekana kwa simu ya mkononi. Wanasayansi wanasema mboga ya mchicha pia inaweza kutumika kufahamu uwepo wa visima vya maji ardhini, kemikali zilizovuja kutoka kwa silaha na madini ya Nitro-aromatics.
Kwa sasa wanasayansi wananuia kuwezesha mboga hiyo kuweza kugundua bomu lililotegwa umbali mrefu ardhini. Tuambie mtazamo wako kuhusiana na hili.
Kumbuka kusambaza makala na pia kuungana nasi kupitia Facebook, Twitter, Instagram, YouTube, Telegram na Google Plus
Chanzo: BBC na mitandao mbalimbali