Huduma maarufu ya mawasiliano ya Zoom yakosekana kwa wengi duniani kote kwa masaa mengi katika tukio linalohusishwa na tatizo la kiufundi.
Huduma ya mikutano kwa njia ya mitandao kupitia video ya Zoom imepata umaarufu na kukua kwa haraka baada ya ujio wa Corona /covid19.
Huduma hiyo inategemewa na maelfu ya watu na makampuni katika kuwezesha mawasiliano na vikao vya kila siku kwa njia ya mtandao.
Upotefu wa huduma hiyo umetokea karibia katika bara yote duniani wateja wa Marekani, Ulaya na ata Afrika Kusini wakiathirika zaidi. Wateja wengi walienda kulalamika mitandaoni hasa hasa kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter kuonesha kutofurahishwa kwao.
Huduma zilizoathirika zaidi ni huduma za vikao vinavyohusisha watu wengi – Zoom Meetings na Zoom Webinars. Huduma zingine kama vile Chat zimeendelea kufanya kazi.
Baada ya masaa mengi ya kufanyia kazi jambo hilo Zoom wamesema tayari huduma hiyo inatakiwa imeanza kurudi kwenye ufanisi kwa watumiaji wake wote.
Everything should be working properly now! We are continuing to monitor the situation. Thank you all for your patience and our sincere apologies for disrupting your day.
— Zoom (@zoom_us) August 24, 2020
No Comment! Be the first one.