Mauzo ya saa janja yaendelea kufanya vizuri mara baada ya kuonekana kuongezeka katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2021 ambapo makampuni makubwa yaendelea kujitutumua.
Mahitaji ya saa janja bado yaonekana kuwa ni kiungo muhimu ambacho kinaingizia makampubi faida kubwa. Hii inachagizwa na ukuaji wa teknolojia ambapo saa hizi zinasaidia katika kufuatilia afya zetu kwa karibu, kuwa mbadala wa simu bila kusahau kutuonya muda ambao daima ni MALI.
Takwimu zinaonyesha hadi katika robo ya pili ya ya mwaka 2021 mauzo ya simu janja yameongezeka kwa 27% huku Apple wakijipatia zaidi ya $100 milioni kutokana na mauzo ya saa janja zao.
Mauzo ya saa janja zaApple yameonekana kushuka kutokana ushindani kutoka kwa makampuni mengine kama Samsung na Garmin ambapo biashara yao ya saa janja imekuwa kwa 43% na 62% katika kipindi cha mwaka hadi mwaka. Galaxy Watch 3 na Watch Active 2 ni saa janja ambazo zimeonekana kuuzika zaidi ingawa hazijafikia umaarufu wa Apple Watch Series 6.
Masoko ya makubwa ya simu janja
Bara la Amerika Kaskazini ndio soko namba moja la simu janja, Uchina ipo nafasi ya pili kwa saa janja kuuzika huko. Mwaka uliopita India ilionekana kuchangia chini ya 2% ya mauzo lakini mwaka huu mambo yamekuwa tofauti kwa kuongezeka na kufikia 6% ndani ya kipindi cha mwaka mmoja tu hivyo kuifanya ndio soko la saa janja linalokuwa kwa haraka zaidi.
Tangu mwaka huu uanze hadi mwezi Agosti mauzo ya simu janja yameongezeka kwa 47% na Huawei wameonekana kutofanya vizuri kama ambavyo takwimu zimeonyesha.
Vyanzo: Counterpoint, Engadget
2 Comments