Soko la saa janja limepanda kwa asilimia 13 toka mwezi Januari mpaka machi 2022. Hii ikiwa ni ongezeko la 13% katika mauzo.
Ni wazi kabisa kwamba saa janja kutoka Apple ndio zilizoongoza kwa mauzo katika mwaka 2021, hii inamaanisha kuwa mpaka sasa bado saa hizo kutoka Apple zipo kidedea.
Taarifa zilizopo ni kwamba inasemekana kuwa saa janja za Apple zimeuza mara 2.5 zaidi ya saa kutoka Samsung (ambao ndio washindani wakubwa)
Kumbuka lakini soko lilishuka sana mwaka 2019 baada ya vizrusi vya CORONA kutawala dunia, mwaka 2020 ndio kidogo kampuni nyingi zilianza kurudisha ukuaji wake wa kimauzo.
Lakini kingine kinachofanya saa janja kutoka Apple zizidi kuwa namba moja ni kwamba wateja wengi wana uaminifu sana na chapa ya kampuni.
Watumiaji wengi wanaotumia vifaa kutoka katika kampuni hii ni vijana na ni moja kati ya jambo linalofanya kampuni kuzidi kufanya vizuri.
Kingine ni kwamba wataalam wanatabiri kuwa thamani ya Apple katika soko la hisa itapanda mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka.
Apple, Samsung, na Xiaomi mpaka sasa ndio wanaongoza katika soko la saa janja dunaini.
Niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, hili umelipokeaje, je na wewe ni mtumiaji wa saa janja?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.