Mpaka kufikia hivi sasa simu nyingi tu zimeshaweza kuruhusiwa kushusha Androi 9 Pie lakini kitu ambacho kinawafanya wateja wa LG kwa upande w rununu kuonekana kuwa nyuma kuhusu kutumia simu zao zikiwa na toleo hilo la kenda kwa mfumo endeshi wa Android.
Ukiangazia kwa jicho la karibu kabisa simu za LG ambazo zina masasisho ya Android 9 utagundua ni chache sanana kwa uhakika kabisa ni wale wenye LG G7 na G7 ThinQ tu ndio ambazo zimeweza kuruhusiwa kupokea sasisho hilo la programu endeshi lakini kwa mujibu wa taarifa kampuni hiyo yenye makao yake Korea Kusini itaruhusu toleo hilo kwenye rununu nne (4).
SImu hizo, LG V30, V30S ThinQ, V35 ThinQ na V40 ThinQ zitaweza kushusha Android Pie mwezi Juni 2019 katika hali ya kujaribu kuwafurahisha watu ambao wanamiliki simu hizo na wamekuwa wakisubiri rununu zao kuweza kuwezeshwa kupakuwa maboresho hayo kwa miezi mingi tuu.