Samsung wameanza mwezi Septemba na masasisho ya kuzifanya simu janja zao mbalimbali ziwe salama ambapo mwezi huu rununu kutoka familia ya Galaxy S20 imepokea vitu vyake.
Kwa watu wenye Samsung Galaxy S20 na nduguze wa familia moja wafahamu ya kuwa masasisho kwa ajili ya kuifanya rununu kuwa salama zaidi kwa maana ya kwamba kuboresha/kuondoa madhaifu yaliyobainika kwenye simu hizo mwezi uliopita yamesharuhusiwa na yapo tayari kupakuliwa.
Samsung Galaxy S20, S20, S20 FE+ na S20 Ultra ni simu janja ambazo zina wateja wengi lakini pia zikiwa ni rununu zinazovutia na tangu kuzinduliwa kwake mwaka 2020 zimekuwa miongoni mwa vivutio vya watu wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani.
Je, unafahamu kuangalia iwapo kuna masasisho yanayohusiana na programu enedeshi kwenye simu janja za Android?
Si kwa simu janja za Samsung tu bali hata nyinginezo inatupasa kufahamu jinsi gani ya kuangalia iwapo kuna masasisho au la! Basi ingia Settings>>Software Update kuweza kujua iwapo yapo au rununu husika bado haijapelekewa zawadi hiyo ya kila mwezi.
Daima ni muhimu kupakua masasisho kwa usalama na ufanisi wa vifaa vyetu vya kiganjani kwani kuma mengi ambayo yanaboreshwa kwenye simu janja na ni muhimu kuyashusha kwenye rununu zetu.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.