Raisi wa marekani Mh. Joe Biden amesaini agizo la kuweza kurusu mitandao (App) ya kijamii mikubwa kutoka china (WeChat Na TikTok) kufanya kazi kama kawaida.
Mitandao ya WeChat Na TikTok mwanzoni ilikua ikiandamwa sana na serikali ya aliekua raisi wa marekani Bw. Donald Trump dhumuni la agizo hilo lilikua ni kukataza kabisa matumizi ya mitandao hiyo marekani.
Serikali ya China imesema hilo ni jambo jema kwani serikali ya bwana Joe Biden inaonyesha dhahiri kuwa serikali hizo mbili zitakuwa katika mahusiano mazuri.
Inabidi ifikie kipindi serikali ya marekani iweze kutoa haki sawa kwa makampuni yote ikiwepo yale ya china hali ambayo itaweza kuepusha ishu za kiuchumi na kibiashara kuibuka baina yao.
Licha ya hayo yote china bado ilisema kuwa likitokea tena kama hili bado yenyewe kama yenyewe itasimamia katika haki na kuhakikisha kuwa inatetea haki zake.
Limekua jambo la kawaida sasa kusikia App fulani imefungiwa katika eneo fulani je hii ni sawa?
Soma Habari Zote Zinazohusu Kufungiwa —> HAPA <—
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Hili Umelipokeaje? Niandikie Hapo Chini Katika Eneo La Comment.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Namba Moja Wa TeknoKona Kila Siku Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!
No Comment! Be the first one.