Kumbuka Meta ndio inamiliki mitandao ya kijamii mikubwa ile ya Instagram, WhatsApp na Facebook. Licha ya mitandao hii kuwa mikubwa lakini bado kampuni imeporomoka kimapato.
Katika robo ya pili ya mwaka inaonyesha kuwa mapato ya kampuni ya Meta yameshuka kwa asilimia 1 ambayo hata hivyo ilikua ni chini kabisa ya matarajio.
Kikibwa ambacho kampuni ilisema ni sababu ya moja kwa moja ni mporomoko wa dili zake za utangazaji, mporomoko wa uchumi na kuongezeka kwa ushindani kutoka makampuni mengine.
Licha ya hayo yote mmiliki wa kampuni hili Bwana, Mark Zuckerberg amesema kuwa kampuni hiyo itajitahidi kufanya mengi makubwa kwa kutumia rasilimali chache ambazo zipo kwa muda huu.
Kingine ni kwamba katika mitandao yote ya kijamii mtandao wa Facebook ndio wenye watumiaji wengi sana ukilinganisha na mitandao mingine, hii inaonyesha hali ni mbaya sana kwani bado hata ukiongezea mapato ya WhatsApp na Instagram bado kampuni haijapata sana…
Kwa kipindi hiki kigumu ni mitandao ya kijamii mingi tuu imekua ikipata mapato ya chini ukilinganisha na ilivyotegemewa
Achana na hawa wamiliki wa Facebook, mitandao kama Snapchat na Twitter na yenyewe imeporomoka kimapato.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je unafikiri kwa kampuni hizi ni nini kifanyike ile warudi katika hali yao ya kawaida?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.