Intel imemteua Bwana. Matt Poirier kuwa makamu wa raisi katika kitengo cha maendeleo ya biashara…..
…kazi hii itaanza rasmi tarehe 30 mwezi huu wa tano. Kwa haraka haraka ni kwamba Kampuni ya Intel imeamua kufanya maamuzi hayo ili kuongeza nguvu (majeshi) katika timu yake.
Kumbuka kampuni ya Intel ni kampuni nguli kabisa katika maswala ya teknolojia za aina mbalimbali.
Wadhifu wa bwana Matt unaenda nyuma zaidi ya miaka 20 na hivyo inamfanya awe na sifa za kutosha katika kazi mpya ambayo ataenda kuianza.
Pia kumbuka kazi hii ambayo anaenda kuianza itakua ni ya kufanya maamuzi ambayo kwa namna moja au nyingine ni ya kuhakikisha timu ya maendeleo ya biashara, inafikia malengo yake kwa kiwango cha hali ya juu sana.
Kwa Uteuzi huu basi hatuna budi kutegemea mabadiliko na maendeleo makubwa kabitika kampuni ya Intel na haswa katika maendeleo ya biashara kwa ujumla.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie umelipokeaje hili katika eneo la comment hapo chini.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.