Urusi wamekuja juu wametoa agizo kwamba kwa makampuni makubwa (ya kiteknolojia) yote ambayo yanataka kuwa yanatangaza urusi kuwa na ofisi kule.
Hali hii inasemekana kuwa itasaidia kwa makampuni hayo kuepukana na kufungiwa baadhi ya matangazo yake na pia kusaidia kuepukana na penati ambazo zinaweza epukika.
Makampuni ambayo yanaguswa moja kwa moja ni yale makubwa kabisa na yanayojihusisha na mitandao ya kijamii. Mitandao kama Facebook, Twitter, WhatsApp, TikTok n.k hii inawahusu sana.
Sheria hii mpya imesainiwa kabisa na raisi wa urusi, Vladimir Putin. Sheria hii ni mahususi kwa makampuni ya kigeni ambayo yanajihusisha na internet kwa namna moja au nyingine.
Kingine ni kwamba kampuni hizo kubwa ni lazima ziwe zinatembelea na warusi zaidi ya laki tano kwa siku ndio sheria hii itaweza kuwagusa.
Urusi ni nchi ambayo kwa kiasi kikubwa inasapoti sana App ambazo zinatengenezwa nchini humo humo, Mwaka 2019 ilitambulisha sheria ya kuamuru watengenezaji vifaa nchini humu kuzalisha vifaa vyao wakati tayari vikiwa vina App za urusi.
Urusi wanajitetea kwa kusema kuwa mitandao hii ikiwa na ofisi nchini mwao inakua ni rahisi kwa wao kuwa na rehani juu yao wakati lolote likitokea
Kumbuka ofisi za Twitter nchini India zilizungukwa na maaskari baada ya kutokea moja ya tweet ya mwanasiasa kudaiwa kuwa picha ambata ilipikwa.
No Comment! Be the first one.