Mwaka huu Xiaomi 12 Ultra itatoka na simu hii inaonekana isiwe tofauti sana ile iliyotoka nyuma yake kwa maeneo mbalimbali yanayopendwa na watu.
Xiaomi 12 Ultra ni simu janja ambayo inazungumziwa kwa wingi na watu wanaofuatilia kwa karibu kutaka kufahamu undani wa rununu husika hata kabla haijatoka. Simu hii ambayo inatazamiwa kutoka kwenye robo ya tatu ya mwaka huu kuna maeneo makuu mawili ambayo yanaelezwa kuwekwa humo. Vipengele hivyo ni:
Kipuri mama
Xiaomi 12 Ultra inaelezwa kuwa na kipuri mama cha uwezo wa juu kutoka Qualcomm na simu hii itakuwa na Snapdragon 8 Gen 1+ badala ya toleo la nyuma yake (8 Gen 1). Kipuri mama hiki kinatajwa kuwa chenye nguvu zaidi kuliko mtangulizi wake.
Kamera
Hili ni eneo la pili ambalo simu hii inatajwa kutokuwa na tofauti na ile iliyotangulia. Simu janja husika inaelezwa kuwa na kamera yenye MP 50 na mbili za MP 48 kila moja sawa kabisa na toleo lililopita (Xiaomi 11 Ultra).
Bado kuna miezi kadhaa ambayo hakika tuyasikia mengi kuhusiana na simu hii. Kwa hivyo vitu vichache tu ni wazi kuwa rununu husika ni ya uwezo wa juu. Tutazidi kukuhabarisha kila machweo na mawio hivyo usiache kutufuatilia.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.