Moja ya sababu ya watu kununua kifurushi cha intaneti ni kuweza kuperuzi mtandaoni halikadhalika kwenye mitandao ya kijamii kwa ujumla wake. Ni wazi kuwa kuna watu wana uraibu wa matumizi ya Instagram lakini ukiwaambia wanaweza wasikubali.
Waliotengenza Instagram walikuja kugundua kuwa mtandao huo wa kijamii unasababisha watu kupata uraibu (addiction) hapa nikiwa na maana ya matumizi ya kitu chochote kupindukia/siku haiwezi kupita bila kutumia ndio tunasema uraibu.
Mwaka 2018, Instagram waliweka kipengele cha “Your Activity” ambacho kazi yake ni kufuatilia muda ambao unatumia kuperuzi kwenye mtandao huo wa kijamii na kwa mantinki hiyo iwapo mtu ameruhusu/amewasha basi atapata taarifa fupi ya kumkubusha apumzike kidogo baada ya kutumia muda fulani akiperuzi kwenye programu tumishi husika.
Sasa katika maboresho ambayo Instagram imeyafanya wamebadili muda wa kukumbushwa kuwa umetumia sana programu tumishi husika kutoka dakika 10 hadi dakika 30 na kuendelea. Hii ikiwa na maana ya kwamba iwapo umechagua kukumbushwa kupimzika kutumia Instagram basi kama zitatimia dakika 30, dakika 45, saa 1, n.k kwa muda wa matumizi ndani ya siku moja basi utapata taarifa fupi ya kukukumbusha upumzike kidogo.
Katika maboresho ya kukumbushwa kupumzika kidogo ule muda ukishafika inatokea bango kubwa mbele ya ukurasa wa programu tumishi husika unaokwambia muda umefika na kama ukiomba kuongezwa muda wameweka ujumbe ule urudi kila baada ya dakika kumi kupita.
Vyanzo: Gadgets 360, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.