Ukitaka kukabiliana na suala zima la uchafuzi wa mazingira basi ni lazima ufikirie kutumia nishati mbadala. Uganda wanaaziwa kuanza kutumia magari yanayotumia umeme wa Jua kabla ya mwisho wa maka huu (2019).
Serikali itaanza kufanyia majaribio mabasi hayo mwaka huu na kwamba serikali iko tayari kutoka shilingi za Uganda bilioni 143 kusaidia utengenezaji wa magari nchini humo.
Mwaka 2014 mamlaka ya uwekezaji ya Uganda ilitoa kandarasi kwa kampuni mbili – Kiira Motor inayomilikiwa na Chuo Kikuu cha Makerere na China Engineering kuanza uzalishaji wa magari mwaka 2018.
Kayoola lina na viti 35 vya abiria pamoja na kuwa na betri mbili; moja inachajiwa kwa umeme Jua na nyingine kwa umeme wa kawaida. Betri inayotumia umeme Jua ikichajiwa itakuwa na uwezo wa kutembea kilomita 80 kabla ya kuchajiwa tena. Aidha, betri nyingine ya umeme wa kawaida itakuwa ni kwa ajili ya matumizi ya safari za usiku.