Hakuna mtu anayependa kwenda sehemu kwa ajili ya kununua tiketi halafu ukatumia muda mrefu kununua tiketi yako ili uweze kusafiri. TeknoKona imekuja na utatuzi wa adha hiyo.
App inayotambukiwa kwa jina la M-Safiri imetenezwa na wanafunzi wa sekondari nchini Kenya, Precious Blood na Riruta wanaofahamoka kama “Team Sniper” walishika nafasi ya pili katika shindano la “Technovation Challenge 2016” lililofanyika San Francisco, California-Marekani.
App hiyo ni mahususi kwa kurahisisha ununuzi wa tiketi za usafiri, kwa magari ya masafa marefu na programu hii inakuongoza hadi kwenye kituo cha basi kwa kutumia teknolojia ya kugundua maeneo (GPS). Badala ya kwenda kupanga foleni, utaenda tu kupanda gari moja kwa moja.
Sababu ya kutengeneza M-Safiri
Harriet Karanja, 16, alikuwa kwenye foleni akisubiri kununua tiketi ya kusafiri kwa basi jijini Nairobi, wakati mama mmoja aliyekuwa kwenye foleni alipokonywa mali yake na wezi na aliposimulia tukio hilo kwa wenzake wanne shuleni, aligundua kwamba pia wao walikuwa wameshuhudia tatizo sawa na hilo. Itakuwaje iwapo tutabuni njia ya kuwaondoa watu kwenye foleni kununua tiketi?
Wasichana hao walipata usaidizi zaidi kutoka kwa walimu, wakufunzi, washauri pamoja na kampuni ya simu ya Safaricom ya nchini Kenya. Baada ya kumaliza masomo yao wasichana hao wana mpango wa kufungua kampuni yao ya teknolojia baada ya masomo ya shule ya upili (sekondari), na pia wanapanga kuisajili programu yao na kuiweka kwenye soko la programu za simu.
Awali wasichana hao walikuwa hawajui jinsi ya kutengeneza programu hizo, kuandika mpango wa biashara ama kuandaa na kuwasilisha wazo la kibiashara.
Lengo kuu likiwa ni kuwapa hamasa wanawake kujiingiza katika masuala ya teknolojia ikiwemo uundaji wa apps mbalimbali na kuongeza motisha kwa watu hasa wanawake kujiajiri. Je, unadhani ni kwa kiasi gani app hiyo itapunguza/kumaliza adha ya kupanga foleni wakati wa kununua tiketi?
Vyanzo: BBC, kachwanywa.com