Kipengele hiki kutoka WhatsApp kimejikita sana kwenye suala zima la ulinzi na usalama katika mtandao huo wa kijamii .
Kitakachokua kinafanyika hapa ni kwamba mtandao huu wa WhatsApp utakua unafanya uhakiki kwa muda huo ambapo mtumiaji anataka kutumia huduma hii.
Hii wanaiita ‘Log in Approval’ nah ii itasaidia sana watu kuweza kulinda akaunti zao maana kwa sasa mtandao umejitanua sana na kama umeweza fuatalia hata watumiaji wa WhatsApp Business watakua na faida kubwa ya kiulinzi na usalama.
Kulingana na taarifa ya chini chini kutoka katika kampuni hiyo ni kwamba kama mtu akiwa anataka kuingia katika akaunti yako basi wewe utatumiwa ombi la mtu huyo kuingia katika akaunti hiyo…hapo unaweza kukubali au kukataa.
Unakumbuka tuliandikia uwezo wa kutumia akaunti moja ya mtandao huo kwenye kifaa Zaidi ya kimoja na hata kwenye huduma ya WhatsApp Business unaweza tumia huduma hiyo kwa kulipia na kupata huduma ya kutumia kifaa Zaidi ya kimoja na hata kuvipa cheo vifaa hivyo
Ngoja Kwanza Soma >>HAPA<< na >>HAPA<< kisha tuendelee.
Mpaka sasa bado hakuna uhakika wa muda juu ya lini kipengele hiki kitawafikia watu na kuanza kutumika lakini kwa sasa kipo katika majaribio.
Ni wazi kuwa WhatsApp (ambao wanamilikiwa na kampuni mama ya facebook,Meta) wanafanya juu chini ili kuhakikisha kuwa wanazidi kubaki kidedea na hii ni pamoja na kuongeza huduma na vipengele kadha wa kadha
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je hili umelipokeaje? Je unaweza kuwa miongoni mwa hao wanaotumia WhatsApp moja kwenye vifaa vingi?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.