Matumizi/teknolojia ya sarafu zisizoshikika imeendelea kuteka hisia za makampuni mengi duniani ambapo kampuni ya Line (inayomiliki programu tumishi ya Line) itazindua sarafu yake ya kidijitali.
Line (kampuni) ni ya nchini Japan ambapo wanatazamiwa kufanya mageuzi kwenye kile ambacho kinawaunganisha kati ya wao na wateja/wananchi wa nchini humo kwa kuzindua safrafu ya kwao wenyewe iitwayo “LINK“.
Safafu hiyo isiyoshikika itatotelwa kama zawadi kwa wateja wanaotumia line kutokana na kutumia huduma mbalimbali zinazopatikana kwenye programmu tumishi husika.
LINK itaweza kutumika kufanya biashara katika mfumo huo wa malipo (BITBOX).
Link itakuwa ni moja ya sarafu za kijitali kama vile vilivyo nyingine; BITCOIN, Munero, n.k.
Ni ukweli usiopingika kuwa teknolojia ya sarafu zisizoshikika zimetokea kupata soko na watu kujipatia kipato kizuri baada ya muda fulani.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|
One Comment
Comments are closed.