Nokia bado haijafa na ipo katika mchaka mchaka wa kuhakikisha kuwa inarudi tena, na wakati huu inakuja kwa kishindo ikiwa inaendeshwa na program Android.
Lakini tukiachana na hilo lingine la kushangaza limetokea, wengi walijua kampuni la Microsoft limesha achana na kuzalisha simu zenye jina la Nokia. Hivi karibuni limetangaza kutoa simu ambazo zina jina hilo.
Simu hizi zinategemewa kuwa ndio za mwisho kutoka Microsoft zikiwa na jina la Nokia. Simu hiyo inakwenda kwa jina la ‘Nokia 216’ na kwa mara ya kwanza itazinduliwa India.
Kmapuni limesema ujio wa simu hiyo mpya ni mzuri tuu licha ya kwamba karibia kila mtu kapagawa na ujio wa iPhone 7.
Simu hii inakuja na kamera yenye MP 0.3 (kwa kamera ya mbele) na kamera ya nyuma inakua na flash. Simu hii kama kawaida itakuwa na FM redio. ‘MP3 player’ kwa ajili ya kucheza miziki na bila kusahau kuwa itakuwa na uwezo wa Bluetooth.
Ukiachana na hayo yote ni kwamba simu hii itakuwa inasapoti teknolojia ya 2.5G tuu katika swala zima la netiweki. Simu hii pia inakuja katika rangi tatu tofauti.
Kama nilivyosema awali, hili bado ni jambo la kushangaza kwani kumbuka bado Mircosoft haijafanikiwa kwa kiasi kikubwa sana katika soko la simu. Ukiangalia simu zao za Lumia na zile za Windows hazikufanya vizuri sana.
Simu hii itazinduliwa mwezi oktoba huko nchini India.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini sehemu ya comment, wewe hii umeipokeaje? Je waachane na mambo ya simu kabisa?.