Ni wiki chache tu WhatsApp iliongeza moja ya maboreaho ambayo kwa maoni yangu naamini watu wengi walifurahia; kuweza kufuta ujumbe ambao uliutuma kwa bahati mbaya au hutaki tena yule uliyemtumia aweze kuuona/kuusoma. Kwa watafiti na wafuatiliaji kama Teknokona mapya yamebainika.
Watu wengi walifurahia sana kwa kile kilichoongezwa kwenye programu tumishi maarufu na pendwa kwa kile ambacho kinaweza kuleta mantiki ya kumuongezea nguvu yule aliyetuma ujumbe husika kwenda kwa mtu mmoja/watu wengi (makundi) na kuweza kuuondoa mara moja pale atakapoona kuwa ujumbe ule haukufaa kumfikia yule aliyemtumia. Swali linakuja hivi inakuaje kama yule uliyemtumia anakuwa na uwezo wa kuuosoma ujumbe ambao wewe ulishaufuta?
Imebainika kuwa ujumbe ambao mtu aliyeutuma na kuuondoa kwenye kumbukumbu za WhatsApp ya kwenye simu janja yake ujumbe aliyeupokea anaweza akauona na kuusoma tena hata bila ya kutumia akili/nguvu nyingi.
Kwa kutumia programu tumishi ya kuonyesha taarifa fupi (Notification) kutoka kwenye Play Store, mtu anaweza akafungua ile taarifa fupi na kuweza kuuona ujumbe ambao aliyeutuma ameufuta na kuweza kufungua na kusoma tena bila ya hata yule aliyeutuma kuwa na taarifa.
Kama mtu akiwa amepakuwa app ya WhatsDelete Pro kwenye simu yake ataweza kupata taarifa fupi iwapo ujumbe fulani umefutwa au taarifa ya kitu chochote cha kwenye simu yake.
App ya Notification History inapatikana kupitia app ya Google PlayStore – WhatsDelete Pro.
One Comment
Comments are closed.