Imedhihirika kwamba maamuzi ya kuunganisha kampuni mbili za Tesla na SolarCity sasa yatafanywa kwa wamiliki wa hisa kupiga kura kuamua kukubali kuunganisha ama kukataa mnamo tarehe 17 mwezi Novemba.
Kampuni hizi zinajihusisha na nini hasa?!
Tesla ni kampuni ambayo inaushawishi mkubwa katika sekta ya magari ya umeme na ambayo yanajiendesha yenyewe wakati kampuni ya SolarCity ni kampuni yenye ushawishi katika sekta ya nishati mbadala. Ni wazi kwamba haya makampuni mawili yataimarika na kuwa na ushawishi zaidi katika sekta hizo kwa miaka ijayo.
Kwanini jambo hili litaamuliwa kwa kura?!
Elon Musk ambaye ni mkurugenzi mkuu wa Tesla lakini wakati huo huo ni mwenyekiti wa Solar City alipendekeza kampuni hizi mbili ziungane mwezi Juni, baadhi ya wanahisa wanapinga mpango wa kuyaunganisha makampuni haya kwa kuwa wanaona mfanyabiashara huyo nataka kujinufaisha na mpango huo hii ndio sababu jambo hili litaamuliwa kwa kura.
Kwa mujibu wa mtandao wa The Newyork Times kila mwenye hisa katika kampuni ya solacity atapata hisa moja kwa takribani kila hisa 10 za SolarCity.
Maamuzi kama kampuni hizi mbili zitaungana yatafikiwa kwa karatasi ya kura ambazo zitapigwa tarehe 17 Mwezi wa kumi na moja.
Endelea kuwa na teknokona kwa habari mbalimbali za Teknolojia katika lugha yako ya kiswahili.