Google wanafahamika kwa vitu vingi ambavyo watu wenye simu za Android wanatumia kwenye vifaa vyao lakini polepole tunaanza kuona programu mbalimbali zikiondolewa kwa maana ya kwamba kutopatikana kwenye soko la programu tumishi/kutoweza kutumika tena na mojawapo ya programu hizo ni Google Allo.
Sisi kama wafuatiliaji wa habari zinazohusu teknolojia tulishawahi kuleta mbele ya macho ya wasomaji wetu kuhusu Allo-programu tumishi iliyomuwezesha mtumiaji kuweza kuwasilianakwa njia ya maandishi/picha jongefu na kupata umaarufu wake lakini sasa Google wameamua kuiondoa kwenye matumizi ambayo haijapokea masasisho tangu mwezi Januari 2018.
Kwanini Google Allo imetolewa?
Wakati inazinduliwa mwaka 2016 lengo la kuleta programu tumishi husika ilikuwa ni kuleta ushindani kwa programu kama vile WhatsApp, Telegram, LINE, Viber lakini mambo yamekwenda ndio sivyo na mwezi Desemba mwaka jana wakaweka wazi Machi 2019.