Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ina nafasi pana tuu katika vita hii dhidi ya virusi vya Corona ambapo jitihada na nguvu nyingi vimewekwa hapa lakini kinachotoka bado kinakuwa na njia mbili!
Mimi kama mwandishi na mfuatiliaji wa habari mbalimbali (ndani na nje ya Tanzania) napata shida sana kujua nafasi ya vyombo vya habari (runinga, magazeti, tovuti, n.k) pale inaposhindwa kutoa kitu kinachostahili. Hili limenikuna na nikiwa sehemu ya vile ambavyo nimevitaja nimeona niliseme. Nimekataa kuchukua njia ya kushoto/kulia ila nasimama palipo sahihi!
Tangu vita dhidi ya virusi vya Corona ni wanahabari/vyombo vya habari vichache sana nchini Tanzania wanaoweza kutambua janga hili kama VIRUSI na SI UGONJWA. Naamini utakubalina na mimi kwamba wengi wao wanavitambua virusi vya Corona kama ugonjwa kitu ambacho si sahihi kumbe ugonjwa wenyewe ni homa kali ya mapafu! Na ndio hapo nasema “KUSHOTO NI TEHAMA halafu kulia kuna VIRUSI VYA CORONA“.
Nini mantiki yake?
Najua wengi wenu mtasema ni namna mojawapo ya kufikisha ujumbe kirahisi kwenda kwa jamii lakini tujiulize Mtanzania huyu akitoka leo akaenda nchi ya jirani na akasema “Ugonjwa wa Corona” badala ya “Virusi vya Corona” ataonekana amekosea ama?. Sisi ambao tunazungumza Kiswahili, tunasikiliza habari kutoka mashirika ya kimataifa mathalani DW Ujerumani, Shirika la Afya Duniani tujiulize tumewahi kusikia wakihabarisha kwa kusema ‘UGONJWA WA CORONA?’.
One Comment
Comments are closed.