Mwanaume mmoja alimshambulia mke wake kwa panga katika kijiji cha Shivakala, Kaunti ya Kakamega, na kumuua kwa kupigiwa simu na mwanaume mwingine usiku wa kuamkia siku ya Jumatatu.
Mwanamke huyo aliyetambuliwa kwa jina la Doreen Masinde, alikimbizwa hadi katika Hospitali ya Rufaa ya Kakamega baada ya kukatwa mkono wa kushoto na mume wake, lakini akafariki kutokana kuvuja damu nyingi.
Mwanaume huyo alishuku kuwa mkewe alikuwa na mpenzi wa kando ndipo akamshambulia na kumkata mkono. Polisi walimkamata mshukiwa na wakapata upanga uliotumiwa katika mauaji hayo.
One Comment
Comments are closed.