iOS 16 iko mbioni kuachiwa rasmi japokuwa kwa sasa kuna toleo la majaribio ambalo kuna baadhi ya watu wanatumia kama sehemu ya majaribio.
Ni wazi kwamba iOS hiyo ina vipengele vingi ambavyo vimeboreshwa na ambavyo ni vipya lakini yote juu ya yote ni kwamba vingi ni vizuri.
Kingine ni kwamba katika ujio mpya wa iPhone 14 basi iOS hiyo itakua kabisa ndani ya simu hizo lakini kwa matoleo mengine ya iPhone kuanzia toleo la iPhone 8 basi watakua na uwezo wa kupata toleo hilo kwa njia ya masasisho (update) kuanzia septemba 12.
Sasa basi turudi kwenye iOS 16 na kujua nenosiri la WiFi
Hapa kabla ya kuendelea inabidi kuna kitu cha kuzingatia na kukiweka akilini, hapa neno siri ambalo litaonekana ni lile tuu la WiFi ambayo awalii ilitumika katika iPhone husika.
Yaani hapa hili litawezekana kama tuu ulishawahi kutumia WiFi hiyo hapo awali katika iPhone yako husika.
Jinsi ya kuwezesha hili ni kwamba inakubidi kwenda katika eneo la WiFi na kisha chagua kile kilama cha bluu pembeni ya WiFi unayoitaka.
Hapo utafunguka ukurasa mwingine na ingia katika eneo limeandikwa Password na kisha tumia Face ID, Touch ID au hata kwa kutumia nenosiri la simu yako
Copy nenosiri (Password) hiyo tayari kwenda kuitumia katika WiFi hiyo ili kuanza kutumia intaneti ya WiFi hiyo.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je unadhani hii ni sawa, maana kuwa wale wengine neno siri la WiFi huwa wanaandika wenyewe kwenye simu zetu ili tusione, vipi hapa?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.