Kodi za wananchi, makampuni, mashirika, n.k ndio zinazoendesha serikali kwenye nchi yoyote ili kuta maendeleo. Makampuni makubwa yanalipa kodi lakini inapobidi inabidi wapandishiwe kiwango.
Sauti ya wengi inaweza kuleta mapinduzi na hali ikabadilika kabisa. Wananchi wa Ufaransa wamekuwa wakiilalamikia serikali kutokana na mambo mbalimbali ambayo hayajawapendeza kitu ambacho kimesababisha maandamano makubwa na hata kushikiza rais wa nchi hiyo ajiuzulu.
Serikali imepata mbinu ya kuwatuliza wananchi wake na hii ni baada ya kutangaza kupandisha kodi iliyoanza kutumika Jan. 1 2019 kwa makampuni makubwa kama Facebook, Apple, Google, Amazon pamoja na mengineyo yanayojihusisha na teknolojia/utoaji wa huduma ya intaneti.
Kiasi cha kodi ambacho makampuni yanajishusha na masuala ya kidijiti nchini Ufaransa.
Ufaransa inatazamiwa kupata $572 milioni kutokana na kodi mbalimbali kwa makampuni makubwa pesa ambazo zitatumika kuhimarisha yale ambayo wananchi wameyapigia kelele.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|