Oppo ni moja ya kampuni ambazo simu zake zinafika sana soko la Afrika na kwa mwezi Mei mwaka huu tayari wameshazindua Oppo K9 ikiongeza idadi ya rununu zilizo na teknolojia ya 5G.
Oppo ambao mara kadhaa wameonekana kwenye orodha ya kampuni ambazo zinafanya vizuri kimaumzo kutokana na bidhaa zao na simu janja wanazozitoa. Leo hii wakati wa kutafuta nini cha kuwahabarisha wasomaji wetu nikavutiwa na sifa za Oppo K9 5G. Je, unataka kufahamu sifa zake? Fuatana nami hadi mwisho wa makala hii. Sifa zake ni hizi:
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.43
- Ubora: Super AMOLED (1080*2400px, 90Hz); ina ung’avu wa hali ya juu sana kufanya kinachoonekana kivutie
Memori :
- Diski uhifadhi: 128GB/GB 256
- RAM: GB 8
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 64, 8 na 2+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 4K na 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 32+uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 4300 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 65W (100% ndani ya dakika 35 tu)
Kipuri mama :
- Snapdragon 768G 5G
Uzito :
- Gramu 172
Programu Endeshi
- ColorOS 11.1, Android 11
Rangi/Bei :
- Nyeusi na Bluu+Kijani+Zambarau
- GB 8/128-$294 (zaidi ya Tsh. 677,948) na GB 8/256-$341 (zaidi ya Tsh. 921,132) bei ya India
Kiujumla ni simu nzuri, yenye kasi lakini pia ina uwezo wa kufanya vingi katika ulimwengu huu wa sasa. Kilichobaki ni wewe msomaji wetu kuamua kama utafanya mpango wa kuiagiza ama utasubiri ifike nchini mwako, jibu unalo mwenyewe.
Vyanzo: GSMArena, Gadgets 360
No Comment! Be the first one.