Wanasheria wakuu wa baadhi ya majimbo nchini Marekani waangalia kama kuna ulazima wa kuilazimisha na kuitenganisha kampuni ya Google na biashara yake ya matangazo ya mtandaoni.
Suala hili linatokana na uchunguzi juu ya shutuma za kujipendelea dhidi ya Google zinazotolewa na makampuni mengine.
Inasemakana kutokana na Google kumilika biashara na mfumo mkubwa wa matangazo ya mtandaoni basi wamekuwa wakizipendelea baadhi ya bidhaa zake hasa hasa katika kutokea zaidi katika huduma ya utafutaji ya Google Search.
Mpango huu umeripotiwa na vyanzo kadhaa na kuthibitishwa na chombo cha habari cha Marekani cha CNBC. Ofisi za Wanasheria wakuu katika majimbo mbalimbali zimeshafungua uchunguzi dhidi ya Google kujipendelea katika huduma ya utafutaji ya Google Search, mfumo wake wa matangazo na kwenye programu endeshaji ya Android.
Msemaji wa Google amesema wanatoa ushirikiano wote unaohitajika na bado wanaendelea na msimamo ya kwamba hakuna upendeleo wowote unaoendelea.
Ni kawaida kwa makampuni yenye biashara nyingi na kujikuta yanaongoza katika kila maeneo yanayojishighulisha kujikuta katika uchunguzi na kesi za kutoruhusu wengine kunufaika na huduma zao. Ata makampuni mengine kama Amazon, Apple, na Facebook wanachunguzwa katika maeneo mbalimbali chini ya sawa la haki za kibiashara za ushindani.