Kuna mengi ambayo yanachapushwa kwenye mitandao ya kijamii ambayo yanaweza kuwa hasi au chanya kulingana na maudhui, jinsi kilivyopokelewa; kusababisha fedheha ama furaha na pengine hata kufikiria kuficha maoni.
Mara kwa mara Instagram imekuwa ikifanyiwa maboresho kulingana na maoni ambayo inapokea kutoka kwa wadau, makosa mbalimbali au jinsi ambavyo inaonekana inapendeza kulingana na mwenendo wa teknolojia kwa wakati huo. Katika kuadhimisha miaka kumi (10) tangu kuzinduliwa kwake, Oktoba 6 2010 programu tumishi husika imeboresha mambo ili kuendelea kuvutia watumiaji wake:
>Mosi, kuficha maoni yanaonekana ni ya kukera. Katika masasisho yaliyowekwa ni maoni yote ambayo yanaonekana yanakera yatafichwa bila ya hata wengine kuweza kuyoaona; jambo hili linafanyika lenyewe tuu (automatically). Hata hivyo, yule aliyeyachapisha kitu kwenye akaunti yake ana uwezo wa kuona maoni yote ambayo yamefichwa.
>Pili, uwezo wa kutangaza biashara kupitia IGTV. Kwa wale ambao tunatumia Instaram kama sehemu ya kutangaza biashara zetu ninaamini kuwa tunafahamu kuhusu kipengele cha IGTV ndani ya programu tumishi husika. Katika maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Instagram, programu tumishi husika imewesha mtu kuweka bei ya vitu kulingana na chapisho lililowekwa kwenye kipengele cha IGTV. Kipengele hikihiki kitaonekana kwenye Reels baadae mwaka huu.
Hao ndio Facebook ambao wanaendelea kuhakikisha programu tumishi inazozimiliki zinaondoloea karaha watumiaji wake hivyo kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kuendelea kuvutia. Kitu cha kufanya ni kupakwa masasisho hayo mapya ili kuweza kufurahia mabadiliko husika.
Vyanzo: TechCrunch, Gadgets 360.
One Comment