Kwenye ushindani wa simu janja Google wameonekana kupata soko zuri tangu ilipoamua kuleta rununu za Google Pixel na tangu hapo wamekuwa wakitoa toleo bora zaidi kuliko lililopipita. Toleo la sasa (Pixel 3 na 3 XL) likiwa halina hata miezi sita sokoni, Google wameamua kukubali ni kweli Google Pixel 3a na 3a XL ndio simu zao zinazokuja.
Kwa wiki kadhaa imekuwepo minong’ono kuhusu Goole kutoa toleo jingine la simu za Pixel na kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa habari za zinazohusu simu janja sina shaka utakuwa umesomasoma mahali. Ndio, na katika hali ambayo haikutegemewa lakini ikiwa kama njia ya kukubali kile ambcho kimekuwa kikisemwa na watu Google kupitia tovuti yao rasmi wakaweka habari kuhusu simu zao na hapo ndipo walipozika minong’ono yote kuhusu Pixel 3a pamoja na vitu vingine ambavyo simu hiyo itakuja navyo.
Kufahamu ujio wa idhaa bila kujua sifa zake huwa haina mashiko sana na kulingana na vyazo vya kuaminika wameweza kuweka wazi sifa kuu za simu hizo mbil ambazo hazipo mbali kuzinduliwa.
Sifa za Pixel 3a (sio rasmi)
Urefu+Ubora wa kioo: inchi 5.6 OLED (1080 x 2220)
Kipuri mama: Snapdragon 670
RAM+Memori ya ndani: GB 4/64GB
Kamera (nyuma): MP 12
Programu endeshi: Android 9 Pie
Nguvu ya betri: 3000mAh
Sifa za Pixel 3a XL (sio rasmi)
Urefu+Ubora wa kioo: inchi 6 OLED (1080 x 2160)
Kipuri mama: Snapdragon 670
RAM+Memori ya ndani: GB 4/64GB
Kamera (nyuma): MP 12
Programu endeshi: Android 9 Pie
Nguvu ya betri: 3000mAh