Mara kwa mara WhatsApp imekuwa ikifanyiwa maboresho ambayo yanatokea kuvutia watumiaji wake kutokana na ukuaji wa teknolojia. Kwa baadhi ya watumiaji wa simu janja wanaweza kuhamisha vitu vyao kwenye WhatsApp kutoka kwenye iOS kwenda Android.
Uwezekano wa kuhamisha vitu mbalimbali kwenye WhatsApp kutoka toleo moja la programu endeshi hadi jingine kwa baadhi ya simu janja huenda hilo likabadilika ndani ya siku za usoni. Ninaposema “Kwa baadhi ya simu janja” namaanisha baadhi ya Samsung Galaxy zinaweza kupokea mazungumzo ya kwenye WhatsApp kutoka kwenye iPhone kwa kutumia waya na programu tumishi-SmartSwitch.
Hatua hiyo ambayo hivi sasa ni ya upande mmoja tu lakini hivi karibuni vimeonekana vielelezo ambavyo vinabainisha kuwa suala hilo lipo mbioni kupatikana kwa watumiaji wote wa WhatsApp. Kwa kile ambacho kimeonekana mchakato huo wa kuhamisha vitu vya kwenye WhatsApp kutoka toleo Android kwenda iOS au kinyume chake utahitaji:
- rununu zote mbili (kwenye Android na iOS) ziwe zina WhatsApp,
- inawezekana ikahitajika waya au WiFi ili kufanikisha mchakato huo.
Mchakato huo kwa sasa bado upo kwenye hatua za majaribio na kielelezo cha hapo juo kimenakiliwa kutoka WhatsApp Beta kwenye iOS toleo namba 22.2.74.
Haijafahamika wazi ni lini kitu hicho kitaanza kupatikana kwa watumiaji wote wa WhatsApp, tukusihi tuu kuendelea kutufuatilia kila leo kwa habari mbalimbali zinazohusu teknolojia.
Vyanzo: GSMArena, WABetaInfo
No Comment! Be the first one.