Serikali imesema haitorudi nyuma udhibiti wa mitandao ya kijamii kwa kuwa na sheria zitakazohakikisha wanakabiliana na maudhi yanayotolewa kupitia redio, na televisheni mtandaoni pamoja na tovuti za kuhabarisha (blog).
Serikali imesisitiza kuwa mitandao ya kijamii itaendelea kudhibitiwa na kamwe haitolegeza msimamo juu ya hilo. Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe mjini Dododma katika hotuba yake wakati wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani.
Dk. Mwakyembe amesema serikali itaendelea kusimamia sheria zilizotungwa katika kuhakikisha wanahabari, waliopo kwenye mitandao ya kijamii wanafanyakazi kwa weledi na kujali maslahi ya taifa na tamaduni za Tanzania.
Vyombo vya kwenye mtandao (TV, redio, mitandao ya kujamii) kwa sasa vimekuwa kama ndio vyombo vikuu na kuna watu wanaamini kila kinachoandikwa mtandaoni ni sahihi hivyo lazima kuwe na udhibiti ili upotoshwaji kwa taifa kuhusu jambo fulani usitokee.