Tangu serikali ya awamu ya sita iingie madarakani nchini Tanzania wimbo umekuwa ni “Kazi iendelee” na namna gani ya kuongeza mapato ya serikali kwa njia mbalimbali kama kukata kodi kwenye maeneo ambayo hayakuwa yameguswa huko nyuma, sasa mitandao ya kijamii inaangaliwwa kwa jicho la karibu.
Teknolojia ina sehemu kubwa katika kufanikisha/kurahisisha vitu mbalimbali duniani kote. Njia ya kutuma na kupokea pesa imerahisisha mambo halikadhalika kuokoa muda lakini pia usalama wa utunzaji wa fedha inakuwa sio rahisi mtu kuibiwa. Hata hivyo, kwa zaidi ya mwezi mmoja (hadi ilipofika Agosti 31) Watanzania walionja shubiri ya tozo kwenye miamala ya simu na kuonekana kuwa si rafiki kwa watu wengi hadi kuifanya serikali kurekebisha vitu; makato/tozo mpya zimeanza kutumika Septemba, Mosi 2021.
Septemba, 1 2021 wakati maelezo ya kina kuhusu marekebisho ya tozo/makato kwenye miamala ya simu yakitolewa Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema yeye na timu yake wanaangalia namna ya kupata kodi kupitia mitandao ya kijamii kama Facebook, WhatsApp, Instagram, Twitter, YouTube, n.k.
Biashara zinahamia kidijitali, kuna ‘Components’ kubwa inayofanya biashara kwa njia za kimtandao. Zile biashara zilizohamia kwenye mtandao hakuna eneo zinazotozwa kodi-Dkt. Mwigulu Nchemba.
Msingi wa hili ni kwamba makampuni makubwa yanapata pesa nyingi kutokana na sisi kutumia programu tumishi, huduma zao, n.k halafu hapa hawana ofisi lakini wanapata kipato na serikali haipati kitu.
Timu ya wataalamu wapo kazini kufikiria namna ya kukusanya kodi kwenye programu tumishi kwa kuangalia nchi mbalimbali wanafanyaje. Haya sasa Mtanzania jiandae kiakili ili hili likija likukute upo tayari.
Vyanzo: Gazeti la Mwananchi, mitandao mbalimbali
One Comment