Kiswahili hivi karibuni kinatarajiwa kuwa lugha ya kwanza kutoka bara la Afrika kutambuliwa na mtandao wa kijamii, Twitter kwa watumiaji wake kote duniani.
Watumiaji wa Twitter duniani kote wataweza kutafsiri taarifa (tweets) zilizowekwa kwa lugha mbalimbali kwenda kwenye Kiswahili ambacho kinazungumzwa zaidi katika nchi za Afrika Mashariki.
Hili limekuja baada ya jukwaa la kwenye mtandao wa kijamii lililoongozwa na watu wa Afrika Mashariki kutaka Kiswahili kutambulika na kuingizwa katika kutafsiri lugha nyingine.
Kufanya ujunbe ufike mbali zaidi, kampeni yenye hashtag #SwahiliIsNotIndonesian na #TwitterRecognizeSwahili imetumika. Kwa muda mrefu machapisho yaliyoandikwa katika lugha ambayo Twitter haiitambui hivyo lugha iliyokuwa inatumika kutafsiri lugha nyingine ni lugha ya Indonesia.
Kutambuliwa kwa Kiswahili kwenye Twitter inakuwa ndio lugha pekee mpaka sasa kutoka bara la Afrika. Twitter inatambua lugha 34 mpaka sasa kutoka duniani kote ambapo awali hakukuwa na lugha yoyote kutoka Afrika.
Lugha za Afrika zimekuwa zikitambuliwa kama lugha ya Indonesia kitu ambacho kimezua kampeni nyingi mathalani #AfricanLanguagesMatter na #AfricanLanguagesDay.