Bw. Andy Yan, Makamu Rais wa kampuni ya Transsion Holdings inayomiliki kampuni Tecno Mobile amesema soko la Afrika ndio kipaumbele cha kampuni yake kabla ya kufikia soko la ulimwenguni kote.
Takribani miaka kumi na miwili (12) iliyopita kampuni ya Transsion ilianza uwekezaji Afrika na siku zote wamekuwa wakiangalia masoko ya Afrika ya kati na Magharibi kwa namna ya pekee kutokana na fursa kubwa iliyoko huko.
Nchi za Ghana na Ivory Coast ni muhimu sana kwa soko la simu za Tecno ambapo kwa nchi ya Nigeria tayari soko kwa upande wa Tecno limeonekana kuwa kubwa na imara katika nchi yenye watu milioni 200.
Bidhaa zao (Tecno) zimeendelea kununuliwa sana Afrika kwa watu wa matabaka tofauti tofauti kwa kuwa bei zao zimekuwa rafiki hata kwa watu wa kipato cha chini. Kadhalika, kuongezeka kwa mapato na kushika soko la simu kwa baadhi ya nchi kadhaa Afrika imetokana na Tecno kuingia ushirikiano na kampuni kadhaa za mawasiliano katika nchi wazouza simu zao.