Apple ambao ndio wanamiliki bidhaa iitwayo AirPods wamekuwa kimya kutoa toleo jipya ya spika hizo za masikioni zisizotumia waya. Kuna kifaa kilichozinduliwa na kampuni nyingine ambacho kinaweza kuchaji AirPods.
Hyper ndio kampuni iliyokuja na kimemeshi ambacho hakitumii waya chenye uwezo wa kuweka umeme kwenye AirPods. Kampuni hiyo si kwamba upo chini ya Apple lakini wanafahamika vyema kwa kutengeneza vitu vinavyoweza kutumika na vya Apple.
Kimemeshi chenyewe kinaitwa Qi ambacho kinachaji AirPods kwa dakika tisini (90) pia kina uwezo wa kuchaji kitu kingine ambacho kinapokea 5W za umeme.
Apple wamekuwa kimya na ukizingatia mpaka sasa Apple hawajatoa bidhaa yenye kutumia teknolojia ya kuchaji bila waya kwenye AirPods. Bei ya Qi ni $50|Tsh. 115,000.
Vyanzo: 9TO5Mac, The Verge
One Comment
Comments are closed.