Nchi ya Kenya imeingia katika vitabu vya historia kwa kurusha Setilaiti yake ya kwanza angani kutokea nchini Japan.
Mapema wiki huu tulileta makala kuhusu Kenya kurusha satelaiti yao kwa mara ya kwaza. Raia wa Kenya walifuatilia tukio hilo moja kwa moja wakiwa mjini Nairobi siku ya Ijumaa.
Satallite hiyo imetengezwa na wanasayansi kutoka katika chuo kikuu cha Nairobi. chuo kikuu kimojawapo cha Italia wakiwa wameshirikiana na wanasayansi kutoka katika shirika la JAXA, Japan.
Kufaulu kwa urushwaji wa satallite hiyo ni faraja kubwa kwa wanasayanzi wa Kenya. Satelaiti hiyo imegharimu kiwango cha fedha zaidi ya dola milioni moja. Nchi zingine za Afrika zilizowahi kurusha satelailaiti zake ni Misri, Afrika Kusini, Nigeria, Morocco na Algeria.