Shirika la Ndege la Kenya Airways limetangazwa kuwa ndio shirika bora zaidi katika uchukuzi wa ndege nchini Kenya kwa matumizi ya teknolojia.
Kenya Airways ilitwaa katika tuzo za Digital Inclusion Awards, 2017 zilizotolewa Jijini Nairobi mwishoni mwa juma. Tuzo hizo hutolewa kwa kampuni ambazo zinatumia teknolojia zaidi katika operesheni zake kwa lengo la kuboresha huduma kwa wateja.
Hii ni kutokana na kuwa kampuni hiyo imeimarisha majukwaa yake ya kielektroniki ya kuwahudumia wateja wake na kuwasiliana nao.