Simu janja ambazo zimeshika hatamu katika teknolojia ya leo lakini pia zinaendelea kuboreshwa kila mara sasa tufahamu ya kuwa siku si nyingi tutaona waya wa kuchajia (USB) wa 240W.
Simu janja nyingi ambazo zimekuwa zikitoka katika miaka ya karibuni zina teknolojia ya kuchaji haraka. Hii ikiwa na maana ya kwamba simu husika inatumia muda mchache sana kujaa chaji kulinganisha na vimememshi ambavyo havina teknolojia ya kuchaji haraka.
Teknolojia iliyopo sasa ina uwezo wa kuchaji kwa haraka kwa nguvu ya mpaka 100W ambayo inafanya vizuri vilivyo kwenye vifaa vya kielektroniki kama simu, kompyuta zinazotumia vipuri mama vyenye nguvu hadi 15W lakini hiyo imeonekana haitoshi hasa kwenye kuchaji ngamizi/ngamizi pakatwa mahususi kwa ajili ya magemu.
Katika kupiga hatua kwenye teknolojia ya kuchaji upo waya wa kuchajia ambao una uwezo wa kuchaji mpaka 240W ambayo inafahamika kwa jina rasmi-USB PD Extended Power Range (EPR) huku umeme unaoingia na kutoka ni 50V na 5A.
Tufahamu kuwa zitakuwepo USB 2.0, 3 na hata 4 ambazo zitakuwa na uwezo wa kuchaji kwa mpaka 240W hivyo basi hatuna budi kuwa na subira tukisubiri ujiowa wa waya wa chaji wenye uwezo kiasi hicho.
Vyanzo: GSMArena, Dignited
No Comment! Be the first one.