Samsung ambao wameendelea kutoa muendelezo wa simu kutoka familia moja na kuwa na kupata mauzo mazuri sokoni lakini mambo si mazuri sana kwa upande wa simu janja za Samsung Galaxy S9 na S9+.
Samsung Galaxy S9 na S9+ hazina muda mrefu sokoni lakini baadhi ya waliozinunua simu hizo wamelalamika kuwa zina matatizo fulani kwenye kioo cha mguso; ukibonyeza kuna maeneo inakubali kufanya kazi na sehemu nyingine hazifanyi kazi.
Tatizo hilo limekwenda mbali zaidi na kwa baadhi ya watu wenye simu hizo wanapta shida sana kuweza kutumia simu hizo kwani upande wa juu kabisa wa kioo wakibonyeza simu inashindwa kwenda kule ambapo mtumiaji amekusudia.
Kwa walio wengi tatizo hilo linaonekana zaidi wakitumia ule mtindo wa “Swipe” au wakitumia keyboard ambayo si ya kweli (virtual).
Kwa wanaopenda kutumia njia ya kufuta kila kitu kwenye simu (factory reset) kama umekumbana na tatizo hili kwenye S9 au S9+ ni vyema ukafahamu haitokuwa suluhisho la kuondoa tatizo hilo kwenye kioo cha mguso.
Vyanzo: Gadgets 360, GSMArena
One Comment
Comments are closed.