Duniani kote wanafahamu moja ya kampuni nguli inajishughulisha na utengenezaji wa bidhaa za kieletroniki ambazo zimekuwa zikiuza wanachotengeza nchi nyingi tuu ulimwenguni, hapa nazungumzia Sony Electronics Corporation.
Sony wamekuwa wakitengeneza vitu vingi ambavyo vimekuwa vikipata soko na kuingizia faida kampuni hiyo ambayo imekuwa ikileta ushindani kwa wapinzani ambao nao wanajihusisha na shughuli hiyohiyo lakini kuanzia Aprili Mosi 2020 kampuni tanzu takribani tatu (3) ambzo zinabeba jina la Sony; namaanisha Sony Mobile Communication, Imaging Products & Solutions and Home Entertainment & Sound. Kwa tafiri isiyo rasmi kampuni hizo tanzu ni ile inajishughulisha na utengenezaji wa simu, kamera na vifaa vya kieletroniki mahususi kwa majumbani ambapo kuanzia tarehe iliyotajwa zitakuwa chini ya mwamvuli mmoja.
Sababu ya uwamuzi huo inaaminika kuwa kampuni hizo zimekuwa zikishindwa kujiendesha vizuri kutokana na kutopata mapato mengi yanayokidhi wao kuweza kujitegemea.
Hata hivyo, Sony Interactive Entertainment amabyo inategeneza Playstations na magemu mbalimbali kutumika kwenye kifaa hicho yenyewe haitaunganishwa na wenzake kwa maana kwamba wao wataendelea kujiendesha kivyao ambao kimsingi wameonekana kuendelea kufanya vizuri kibiashara.
Maamuzi ya kuzileta kampuni tatu za Sony sehemu moja yanalenga kuziongezea mauzo/uwezo wa kujitangaza, kupata wateja, n.k na hatimae kuifanya kiongozi mkuu anayezibeba zote kujiongezeaa mapato. Je, wewe ni shabiki wa bidhaa za Sony?
Vyanzo: GSMArena, SRN