Kampuni ya Hewlett-Packard maarufu kama HP kwa mara nyingine tena imeendelea kuongoza katika ufalme wa soko la Kompyuta duniani.
Makampuni mawili ya utafiti wa soko la teknolojia, IDC na Gartner wote wanakubaliana kwamba HP kwa sasa ndio inashikilia soko la kompyuta duniani.
Kampuni ya utafiti ya Gartner ilisema Lenovo imeongoza kwa mauzo katika robo ya pili na kwa mujibu wa IDC robo ya kwanza iliongozwa na HP.
Kampuni ya HP yenye makao makuu yake California, nchini Marekani kwa mujibu wa utafiti uliotolewa na Gartner mauzo yake yamekuwa yakipanda mwaka baada ya mwaka katika uuzaji wa kompyuta zake.
Uongozi wa HP umekuwa mashakani kwa kukabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa Lenovo. Utafiti huu unasema kufikia mwisho wa mwaka kunaweza kutokea mabadiliko ya kampuni yoyote kati HP na Lenovo kuongoza.
Hata hivyo kampuni ya Gartner imesema jambo la kutisha ni kwamba mauzo ya kompyuta yameendelea kushuka mwaka hadi mwaka ambapo mauzo ya robo ya kwanza kwa mwaka huu duniani kote ziliuzwa kompyuta milioni 61.1.
Kampuni hiyo ya utafiti ya Gartener imesema kushuka kwa soko la uuzaji kompyuta kumesababishwa na uwepo wa nguvu wa Simu janja (Smartphone) na Tablets.
Na pia kumbuka ya kwamba ni kawaida mtu kutumia kompyuta ile ile kwa miaka mingi zaidi bila uhitaji wa kubadilisha wakati kwenye eneo la simu wengi wao hubadilisha mara kwa mara.