TECNO kama kawadia yao, wamekuja na kingine kipya, mara hii wamekuja na simu mpya ya TECNO Camon 15. Inajulikana wazi kuwa simu zao za matoleo ya camon zimejikita sana katika teknolojia ya picha.
Simu inakuja na kamera nne (4) ni simu chache sana sasa hivi ambazo zinakuja katika mfumo huu wa kamera. Najua una shauku ya kutaka kujua mfumo wa kamera wa simu hizo, leo TeknoKona tunakufahamisha kuhusiana na hilo.
Kamera Kuu: mfumo wa kamera nne huku kamera kuu ikiwa na MP 48, Kamera mbili zikiwa na MP 2 , na ya nne ikiwa na lenzi ya QVGA. Mfumo huu pia unasapoti kurekodi video zenye ubora wa 1080p ambayo ni fremu 30 kwa sekunde.
Kamera Ya Mbele: MP 16 ikiwa ndani ya kioo cha LCD. Kwa teknolojia ya sasa ni kawaida kabisa kwani kwa sasa simu nyingi zinakuja huku kamera yake ikiwa ndani ya kioo.
Ukiachana na ukubwa katika swala zima la megapixels katika simu hii bado kamera zake zinaweza fanya mambo mengi sana ukilinganisha na kamera za simu zingine.
Vilevile, kuna teknolojia ya kwanza kabisa kutoka TECNO ambayo inaweza kupiga picha katika mazingira ya giza kali tuu bila kutoa flash na picha ikatoka na mwanga wa kutosha (fikiria kupiga picha usiku wa manane) vile vile kamera ina vitu kibao kama vile AI (Artificial Intelligence) katika kamera yake.
One Comment
Comments are closed.