Hatujapata masasisho (update) kwa simu za iphone 6 kurudi chini kwa muda mrefu sana sio? Sasa Apple imeona ilete sasisho katika baadhi ya matoleo katika simu hizo.
Toleo la program endeshi ambayo imepewa uwezo wa kuwa na sasisho jipya ni iOS 12, ahahaha najua ni kitambo sana hii lakini hata hivyo sio kwa vifaa vyote vya iPhone
Watumaiji wengi wa iPhone watakua wameshasahu toleo hili kwani kwa sasa linategemewa kwa hamu ni toleo la iOS 16 ambalo kwa sasa lipo katika majaribio lakini litatoka hivi karibuni ndani ya mwezi huu wa 9.
Unaweza ukawa unajiuliza sasisho hilo litakua linaambatana na vitu gani? Jibu ni kwamba watumiaji wote ambao wanatumia simu za iPhone 5S, 6 au 6 Plus basi wataweza kupata sasisho ambalo ndani yake limejikita katika ulinzi na usalama.
Ili kuwezesha hili ingia katika Settings > General > Software Update. Na kasha fuata hatua zitakazotokea moja baada ya nyingine.
Toleo hili la sasisho pia litaweza kuingia katika baadhi ya vifaa vya iPad ambavyo ni iPad Air, iPad Mini 2 na 3 tuu.
Ni mara chache sana kwa kampuni ya Apple kurudi nyuma na kuanza kutoa masasisho kwa vifaa vyake vya nyuma ambavyo kwa sasa sio kipaumbele kabisa katika kampuni
Ningependa kusikia kutoka kwako, je unatumia baadhi ya vifaa hivi au umeshaachana na hayo matoleo uko katika matoleo ya juu zaidi?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.