Serikali ya China kupitia jeshi lake la Polisi wamefunga zaidi ya kamera milioni 176 kwenye maeneo mbalimbali nchini humo ili kuweza kukabiliana na matukio ya kihalifu kabla hayajatokea.
Kamera hizo pamoja na kompyuta zenye weledi wa hali ya juu (Artificial Intelligence) zitaweza kutambua sura za watu na kitu wanachotaka kufanya kabla ya wao hawajatimiza dhima la kufanya tukio hilo.
Jinsi kamera hizo zinavyofanya kazi.
Kamera zitakuwa zinachukua matukio ya mtu kisha kompyuta itaweza kuchanganua matendo yake na kuweza kubainisha yenyewe kama huyo mtu ni muhalifu au si mhalifu na kama ikigundua ni mhalifu basi kompyuta itatoa taarifa polisi haraka sana ambapo wao polisi wataweza kukabliana naye kabla hajafanya tukio.
Kwa mfano mtu akionekana kwenye kamera anakwenda kununua kisu dukani hatotiliwa mashaka na kompyuta hizo, ila mtu huyo huyo akionekana tena karudi kununua nyundo na gunia basi kompyuta itatoa taarifa polisi ili mtu huyo aweze kufuatliwa kwani inawezekana anataka kwenda kufanya mauaji.