Katika njia mojawapo ya kufanya mawasiliano na mtu yeyote na popote duniani ni kwa kutumia na barua pepe. Mbali na hilo matumizi ya simu janja ama vifaa vya kidijiti linafanya mtu aweze kutuma jumbe kwa urahisi na haraka zaidi.
Kutokana na ukuaji wa teknolojia ambapo mtu anaweza akawa anatumia barua pepe (Yahoo, Hotmail, n.k) tofauti na Gmail lakini uwepo wa simu janja hasa za Android zimelazimisha watu kuwa na akaunti kwenye Gmail. Na ukiwa kama mtu ambae unatumia barua pepe kufanya mawasiliano mara kwa mara, kuifanya ionekane kuwa nadhifu na rasmi ni muhimu ukafahamu jinsi ya kutumia ama kuweka saini kwenye akaunti yako ya Gmail.
Fuata njia hii kuweza kuweka saini kwenye barua pepe (Gmail)
>Hatua ya kwanza kabisa ni kuingia kwenye akaunti yako ya Gmail kisha nena kwenye mpangilio (settings) kisha bofya “See all settings“. Kuna ukurasa mdogo utafunguka sasa shuka shuka chini mpaka utakapoona neno “Signature” halafu bofya “Create new“.

>Andika jina unataka kuita faili ambalo ndani yake ndio utaweka vitu ambavyo vitasimama kama saini yako kwenye barua pepe. Kumbuka: Jina hili linaweza kuwa barua pepe ama neno lolote utakalopenda kuweka. baada ya hapo bonyeza “Create“.

>Sasa andika vitu ambavyo unataka saini yako iwe navyo kwa maana ya kwamba inaweza kuwa jina lako, cheo, anwani, tovuti, n.k. Vilevile, inawezekana kuweka picha ya kitu chochote. Hapa utabonyeza sehemu ya kuambatanisha picha (images).

>Ili kuweza kufanya saini iweze kuonekana ni lazima uchague ionekano wakati gani na kwenye akaunti ipi (kama unatumia barua pepe ambazo zote unazitumia kupitia Gmail). Baada ya hapo shuka chini kabisa na bofya “Save changes“.

>Inawezekana kutengeneza saini nyingi tuu na kuzipa majina tofauti tofauti na kuzitumia kadri ambavyo utakuwa umechagua ipi ya kutumia kwa wakati huo.

Kwa maelezo hayo nina hakika kabisa utaweza kufanya kila mara utakapokuwa unafanya mawasiliano kwa njia ya barua pepe. Tunakaribisha maoni yenu wasomaji wetu.
Chanzo: Mail Signatures
One Comment
Comments are closed.