Hivi unajua kuna baadhi ya sehemu duniani watu wana jina moja tuu. Angalia Indonesia watu wengi wanatumia jina moja tuu. Hii inamaanisha nini? hawana baba?. Facebook wametoa ruhusa kwa watu wa indonesia kutumia jina moja tuu.
Makala hii itakufundisha wewe mtu wa eneo lingine (sio indonesia) kutengeneza jina moja katika mtandao wako wa kijamii wa facebook. Kabla ya kwenda moja kwa moja kwenye makala kwanza inakubidi ujue kuwa facebook hawajaruhusu njia hii lakini TeknokonaDotCom inajitolea kukufundisha maujanja haya.
- Njia Za Kufuata Ili Kuwa Na Jina MojaKwanza kabisa log in katika mtandao wako wa facbook
- Wakati uko ndani ingia katika Account Setting kisha badilisha lugha kuwa Bahasa Indonesia.
- Sasa Baada ya hapo inabidi uwafanye Facebook wakuamini kuwa uko Bahasa Indonesia na unaishi huko. Utafanyaje hilo?
Njia Ya kuwafanya facebook wakuamini kuwa unatokea Bahasa Indonesia. inakubidi ufanye hili lifuatalo
Ingia katika mtandao wa http://www.proxynova.com/ na kisha nenda katika sehemu ya Proxy Server List na kisha chagua indonesia au kwa urahisi bofya hapa kisha kopi Proxy (Proxy IP na Proxy Port) yenye spidi kubwa kuliko zote katika list iliyotokea.
- Kisha bonyeza Kibonyezo cha Alama ya Window + R katika keyboard ya kompyuta yako ili kuiita Run. Ikitokea Run Andika inetcpl.cpl kisha bofya Enter.
- Kuna Kiboxi kitatokea na kikishatokea nenda katika settings na kisha nenda katika Local Area Network (LAN). Click katika Connections na kisha
- Weka alama ya tiki katika ‘Use Proxy Server for your LAN’ Kisha paste Proxy (Proxy IP na Proxy Port) katika eneo la address (zile ulizozikopi hapa)
Muhimu: Usingali proxy zilizopo katika picha hapo juu. Kila mara tegemea zile mpya katika mtandao
- Ukishamaliza bonyeza Ok. Sasa jaribu kubadilisha jina lako kama kawaida tuu unavyofanyaga. Andika jina la kwanza sehemu ya kujaza la pili na la tatu iache wazi kisha ingiza neno siri lako. Hifandhi marekebisho (save settings)
Safiiiiiiii! Facebook wamekubali mabadiliko ya jina lako sasa
Baada ya jina lako kubadilika sasa badilisha settings za Proxy ili ziwe kama mwanzo kabisa. Hiyo ni kuondoa Proxy uliyoweka katika LAN yaani
- Bonyeza Kibonyezo cha Alama ya Window + R katika keyboard ya kompyuta yako ili kuiita Run. Ikitokea Run Andika inetcpl.cpl kisha bofya Enter.
- Kuna Kiboxi kitatokea na kikishatokea nenda katika settings na kisha nenda katika Local Area Network (LAN). Click katika Connections na kisha futa proxy ulizoziweka mwanzo na kuacha eneo hilo la address wazi bila kujaza kitu, baada ya hapo ondoa alama ya tiki katika ‘Use Proxy Server for your LAN’ kisha bofya okay
- Ukimaliza hayo yote inabidi urudi FB na ubadilishe lugha yaani kutoka Bahasa Indonesia kwenda lugha unayotaka ambayo utatumia bila shaka
No Comment! Be the first one.