Kama zilivyo simu janja zetu tunaweza vile vile ku’screen shot’ hata ‘screen’ ya kompyuta zetu. Ni wazi kuwa kuna muda tunataka kuchukua baadhi ya taarifa fulani katika kompyuta na kunakili tukio husika katika kompyuta ikawa ndio njia rahisi kabisa
Leo TeknoKona inakuletea njia mbili za kuwezesha kulifanya hilo. pengine itategemea ni njia gani rahisi kwako ambayo utaweza kuitumia.
NJIA YA KWANZA
Njia ya kwanza ambayo imezoeleka na wengi ni ile ya kubonyeza vibonyezo vya ‘FN + Prt SC’ kwa wakati mmoja. Baada ya kubonyeza vibonyezo hivyo hapo utakua umenakili chochote ambacho kilikua katika ‘Screen’ ya kompyuta yako.
Lakini hapo bado utashindwa kukiona cha kufanya basi ni kwenda juu ya picha yeyote na kisha ‘Right Click’ na kisha nenda sehemu ya Edit. Ikifungua nenda sehemu ya ‘File’ na kisha nenda katika sehemu ya ‘New”
Ukurasa mpya ukifunguka cha kufanya ni kubonyeza ‘Ctrl + V’ kwa wakati mmoja na hapo utakuwa umeweza kuiweka ile nakala yako pale
Cha mwisho kufanya hapo ni kwenda sehemu ya ‘File’ na kisha u ‘Save’ kazi hiyo katika mfumo wa picha za kawaida (GPJ). Mpaka hapo utakua umefanikisha hilo
NJIA YA PILI
Njia hii itawezeshwa kwa kutumia ‘Snipping Tool’
Kuliwezesha hili itakubidi ubonyeze alama ya ‘Windows’ katika ‘Keyboard’ ya kompyuta yako na kisha uandike neno ‘Snipping tool’, likitokea boonyeza ili kuifungua.
Ikifunguka bonyeza sehemu ya ‘New’ ili kuanza kuitumia
Bonyeza mwanzo wa eneo unalotaka kulichukua bila kuachia ‘Mouse’ shuka mpaka chini mwa eneo hilo na kisha achia ‘Mouse’ (Drag) baada ya hapo ‘Snipping Tool’ itafunguka na kuonyesha eneo ambalo umelichagua.
Baada ya hapo bonyeza sehemu ya ‘File’ na kisha ‘Save’ File hilo kama picha katika eneo unalolitaka
Mpaka hapo utakua umeshafahamu njia hizi mbili. cha msingi ni kuchagua ile moja ambayo unaiweza zaidi na kisha kuanza kuitumia.
Njia Hizi Zitatumika VIzuri Kwa Watumiaji Wa Windows!
Usisahau kutembelea mtandao wako pendwa wa TeknoKona kila siku kwa habari moto moto zinazohusu Teknolojia kwa ujumla.