Google wanazidi kuleta maboresho kadha wa kadha kila siku, hii ni katika hali ya kujihakikishia inaendelea kujiboresha zaidi.
Mtandao wa Google ndio mtandao ambao unaongoza kutembelewa kwa siku, watu huenda ili kupata taarifa mbalimbali za matafuto (search) yao.
Taarifa ambazo huwa zinapatikana hapo ni za aina mbali mbali kwa mfano ingia HAPA ujionee kuhusiana na TeknoKona. Taarifa hizo huwa zinabeba vitu vingi, kwa mfano taarifa za watu kama vile namba za simu, taarifa z akibenki n.k
Vi Google imeboresha sera zake hasa kwa kipengele cha personally identifiable information (PII) ambapo humu kuna ulinzi ambao unaweza zuia hata wizi wa utambulisho n.k
Sasa Unaweza Kuzuia/Kuondoa Taarifa Hizo.
Anza Kwanza kwa kuweka ombi lako HAPA, Ukiingia hapo ukurasa mpya utafunguka na itakulazimu kujaza baadhi ya taarifa na kisha Google wenyewe wataangalia kama taarifa hizo zinakidhi vigezo vya kuondolewa.
Kama kweli ukifanikiwa basi mtandao wa Google utazuia taarifa hizo kuondokea kwenye majibu ya matafuto (Search) yake, kwa mfano mtu akiandika jina lako katika mtandao wa Google.
Kingine cha msingi cha kufamu ni kwamba, sio kama mtandao wa Google utazifuta taarifa hizo kabisa. hapa kinachofanyika ni kwamba Google inakua haizileti taarifa hizo katika majibu ya matafuto yake (search result).
Ili taarifa ifutike kabisa inabidi mtandoa husika ufute taarifa hiyo.
Ningependa Kusika Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Uwanja Wa Maoni
Tembelea Mtandao Wako Pendwa Wa TeknoKona Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
No Comment! Be the first one.