Google Drive ni njia moja wapo na maarufu sana ya kuhifadhia taarifa (picha, video, nyaraka n.k) katika mtandao.
Hivi karibuni niliandika pia kuhusiana na Google Docs kupata sasisho jipya ambalo halina utofauti mkubwa sana na hili.. Ingia HAPA ili kusoma hilo.
Google kwa sasa kupitia Google Drive wameweka/wameongeza kipengele cha uwezo wa kukata (cut), kunakili (copy), na kuweka nakili hiyo (paste) katika mtandao huo kwa kutumia njia za mkato za keyboard.
Kwa haraka haraka ni kwamba ili kuweza kufanya hivyo inabidi uwe unatumia huduma hiyo kupitia kivinjari cha chrome?
Google wenyewe wanasema kila mtu ataweza kuwa na uwezo wa kutumia kipengele hichi mpaka kufikia juni 4.
Hapa ni kwamba utakua na uwezo wa kutumia njia hizo za mkato katika Google Drive kama ulivyokua unazitumia katika kompyuta yako kawaida.
Kumbuka kwa Windows na Mac tunatumia vibonyezo vya kawaida ambavyo ni Control / Command + C, X, na V katika kuhakikisha tunafanikisha kunakili, tunakata au tunaweka nakala za machaguo yetu.
Najua inaweza ikawa ni vigumu kuamua kuwa mpaka sasa huduma hii haikuwepo katika mtandao huo, ila uzuri ni kwamba kwa sasa unaingia sio?
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, Hii umeipokeaje?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.