Unaweza ukawa unatumia kompyuta ambayo kihifadhi data hakijagawanywa. Je, unajua kuwa ni hatari kutumia kompyuta ambayo diski huifadhi haijagawanywa? Pata kufahamu kutoka kwetu, TeknoKona.
Ni muhimu sana kuhakikisha kuwa kompyuta unayotumia hard disk yake imegawanywa na hili kuweza kugawanya hard disk (HDD) ya kompyuta yako ni muhimu kufuata hatua zifuatazo:-
- Fungua Disk Management kwenye komyuta. Kwa urahisi unaweza kufungua kwa kutumia ‘Run‘ (bonyeza kitufe cha ‘Windows+R‘) kisha andika ‘diskmgmt.msc‘.
- Bonyeza sehemu iliyoandikwa “Unallocated” (ina ufito mweusi) kisha chagua New Volume ili kuweza kutengeneza partition mpya kwenye HardDisk. Pia kama diski nzima ni Drive C na unaona bado ina nafasi nyingi ambayo inaweza ikatosha kuwa nafasi mpya basi ichague kisha bofya Shrink.
- Weka kiasi ambacho unataka partition unayoitengeneza kwenye kihifadhi data kwenye kompyuta yako kiwe nacho. Kisha bonyeza Next.
- Chagua herufi ambayo unataka partition yake iwe nayo. Inaweza kuwa herufi E, F, H lakini sio herufi C kisha bonyeza Next.
- Unaweza kuchagua kufuta (format) kila kitu kwenye ile sehemu ya hard disk unayoitengeneza. Kufuta chagua ya pili katika orodha na kama hutaki kufuta kila kitu basi chagua ya kwanza katika orodha halafu bonyeza Next.
- Bonyeza Next kuweza kumaliza mchakato mzima wa kugawanya kihifadhi data katika kompyuta yako. Kisha bonyeza Finish kama ishara ya kukamilisha mchakato mzima wa kutengenza parttion.
Kwa hatua hizo kwa hakika utakuwa umewza kuigawanya diski uhifadhi na kutokana na maombi ya wasomaji wetu, kutaka kujua jinsi ya kuigawanya kihifadhi data, TeknoKona imeitika ombi na imewajuza.
Imeandikwa kwa kutokana na ujuzi binafsi pamoja na picha kutoka TechNet Magazine