Nikikumbuka miaka ile nipo chuo nikipata elimu ya taaluma hadi leo bado simu janja Sony Xperia zipo na zinaendelea kutoka tuu na kubwa zaidi wanasifika sana kwa kuwa na kamera nzuri.
SIku zote simu za Sony Xperia zimekuwa zikinivutia kila moja ambayo inatoka na kadri ambavyo teknolojia inakuwa ndio zinazidi kuvutia jicho la mwandishi. Karibu na mwisho wa mwezi Oktoba mwaka huu Sony Xperia Pro-I ilizinduliwa na kama kawaida yetu TeknoKona tuileta mbele ya macho ya wasomaji wetu kwa maana ya uchambuzi wake.
Muonekano|Uwezo wa simu
Kwenye dunia ya leo makampuni mengi yanatengeneza simu janja ambazo zina kioo kipana kwa lengo la kuvutia jicho la wateja. Sony Xperia Pro-I ina kioo chenye urefu wa inchi 6.5, ubora wa OLED na pande zote (mbele/nyuma) inalindwa na kioo cha Gorilla Glass. Hii ni simu ya 5G ambapo nyuma ya pazia inawezeshwa na Snapdragon 888 5G.
Kamera|Betri
Sehemu mojawapo ambayo Sony huwa wanawaacha watu midomo wazi ni kwenye kipengele cha kamera kwani sifa zake zinaweza kuwa za kawaida (hautishi) ila kinachotoka hapo ni kizuri kweli. Simu hii ina kamera ina kamera 4; tatu zina MP 12 na moja ina MP 0.3 lakini ubora wake unatofautina kwenye uwezo wa kukuza vitu (picha) pamoja na mambo mengine.
Memori|Sifa nyingizo
Nguvu nyingine kwenye Sony Xperia Pro-I imewekwa kwenye memori; ina RAM 12 GB, 512GB za diski uhifadhi lakini pia ina nafasi ya kuweka memori ya ziada. Ina sehemu ya kuchomeka spika za masikioni, uwezo wa kutoingia maji/vumbi hadi umbali wa 1.5m kwa dakika 30, inatumia Android 11.
Kwa wapenzi wa simu nzuri kama Sony Xperia Pro-I na hasa ukizingatia uwezo wa kamera lakini pia kuhifadhi vitu (memori) simu hii ni chaguo sahihi ambayo bei yake ni $1,798|zaidi ya Tsh. 4,144,390 kwa ughaibuni.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.